Mgeni wetu ni mratibu wa mkoa wa Mradi wa Uimarishaji na Ufufuzi Mashariki mwa DRC, STAR-EST huko Kivu Kaskazini. Atatueleza kuhusu misheni yake ya wiki mbili katika jiji na tarafa la Beni ambayo ilikuwa ya utambulisho wa miradi ya msingi ya kijamii na kiuchumi itakayofadhiliwa, hususan ujenzi wa shule za umma, vituo vya afya na ujenzi wa chem chem za maji ya kunywa na ukarabati wa baadhi ya barabara za mijini na zile za huduma za kilimo katika mji na wilaya ya Beni. Jean-Claude Kasomo, mratibu wa mkoa wa STAR – EST ??katika Kivu Kaskazini, anazungumza kuhusu mada hii na Marc Maro Fimbo.

Source: Radio Okapi

By admin